Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Estominh F. Chang'ah akipokea kitambulisho cha Taifa kama ishara ya Uzinduzi wa ugawaji wa vitambulivyo hivyo akiwa na Shahidu D. Mrabyo. |
Mkuu
wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Estominh F. Chang’ah amezindua rasmi zoezi la ugawaji
wa vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa watumishi wote wa Serikali walio
andikishwa Wilayani Ukerewe. Uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi mkubwa wa
Halmashauri ambapo amepongeza zoezi limefanikiwa kwa asalimia 97%.
Kitambulisho kitarahisha huduma mbalimbali na kuongeza maendeleo na kupunguza
urasimu na itasaidia hata kwa watumishi watakao hitaji mikopo ya kufanya
shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
Shahidu D. Mrabyo Afisa Msajili (W) akiongea na watumishi wakati wa Uzinduzi |
Shahidu D. Mrabyo Afisa Msajili (W),
ameeleza kuwa zoezi la uandikishaji lilianza tarehe 3/4/2016 na Katika zoezi
hilo jumla ya watumishi waliotakiwa kusajiliwa ni 3103 lakini watumishi 2932
walitambuliwa na kusajiliwa na maafisa wa NIDA kwa kushirikiana na Uongozi
husika wa mashirika au Taasisi za serikali, na watumishi 81 walikua tayari wamekwisha sajiliwa sehemu mbalimbali nchini na
hivyo kufanya idadi ya wanaotakiwa kuwa na vitambulisho kuwa 3013 na hivyo kufanya zoezi hili
kufanikiwa kwa 97.099%.
Watumishi wa Serikali katika ukumbi wa Halmashauri wakati wa uzinduzi |
Vitambulisho vinatengenezwa kwa awamu
mbili, vitambulisho 2932 vilivyoombwa,
kwa awamu ya kwanza ni vitambulisho 2519
vipo tayari kwa kugawiwa sawa na asilimia 85.91
na vilivyobaki vitakuja katika awamu nyingine.
Kitambulisho cha Taifa kina uwezo mkubwa
wa kufanya kazi nyingi kwa pamoja, huko tunako elekea katika teknolojia
kitatumika kama kitambulisho cha Taifa, kitatumika kupigia kura, kitatumika
kama kadi ya mfuko wa hifadhi ya jamii, leseni ya udereva, passport ya
kusafiria, pia itakuwa ni kadi ambayo unaweza kuhifadhia fedha na kuitumia
popote kwa kuchanja tu, pia inaweza kutumika kama kadi ya kuingilia uwanjani
mf. Uwanja wa Taifa, tutaweza kuitumia kupanda magari ya mwendo kasi na
matumizi mengine mengi kulingana na kadri itavyokuwa inaunganishwa na mifumo
mbali mbali hapa nchini.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Song'ora J.K Nyango akipongeza hatua ya ugawaji wa vitambulisho kwa Watumishi wa Serikali |
Zoezi linalofuata na ambalo limekwisha
anza ni uandikishaji wa wananchi wote ambapo mpaka sasa fomu za usajili
zimekwisha sambazwa katika kata zote za Tarafa ya Mumbuga ambazo ni Bukongo,
Nkilizya, Kagera, Nansio, Kakerege, Nakatunguru, Bukanda, Namagondo na Ngoma.
Ametoa rai kwa wakazi wote wa tarafa ya Mumbuga kwenda kuchukua na kujaza fomu
na kuwa na viambatanisho vingi iwezekanavyo ilikurahisisha upatikanaji wa
kitambulisho, viambatanisho vinavyohitajika ili kusajiliwa ni cheti cha
kuzaliwa, vyeti vya elimu, kitambulisho cha kupiga kura, kitambulisho cha bima
ya afya, kitambulisho cha mfuko wa hifadhi ya jamii, TIN namba, kopi ya
kitambulisho cha taifa cha mzazi.
Kuhusu mwanachi atakayepoteza
kitambulisho cha Taifa atalazimika kulipia Tshs. 20,000/= kwa ajili ya kupata
kingine, pia tunatarajia kuanza kusajiri wageni wanaoishi kihalali katika
maeneo yetu, kwa hiyo ni vyema kama wapo wakaja kutuona kwa ajili ya kusajiliwa
kama wageni.
Mrabyo amemshukuru
Mkuu wa Wilaya, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya
Wilaya ya Ukerewe, wakuu wa idara mbalimbali, wakuu wa taasisi mbalimbali za
Serikali na watumishi wote wa Serikali Wilayani Ukerewe.
Shahidu D. Mrabyo akimkabidhi kitambulishi cha Taifa Hakimu Mfawidhi (W) Francis Kishenyi |
Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe na baadhi ya wakuu wa idara na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya katika picha ya pamoja. |
No comments:
Post a Comment