Mkurugenzi Mkuu wa Rex Energy Bw. Francis Kibhisa akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa umeme jua kisiwa cha Gana |
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Bw. Frank S. Bahati akizungumza katika uzinduzi wa umeme jua kisiwa cha Gana. |
Wananchi
wanaoishi maeneo ya visiwani wilayani Ukerewe wanatarajia kunufaika na huduma
ya nishati ya umeme. Nishati hiyo ya umeme jua inayowezeshwa na mwekezaji Rex
Energy ambao unatakuwa ni moja ya kichocheo cha uchumi wa maeneo mengi ya
visiwa katika wilaya ya Ukerewe na hii
ni baada ya kufanya uzinduzi wa mradi huo wa umeme katika kisiwa cha Gana,
uliohusisha wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia tukio hilo
lililoongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Frank
S. Bahati na Mkurugenzi mkuu wa Rex Energy Francis Kibhisa ambaye ndio
mwekezaji.
Uwekaji saini katika uzinduzi wa mradi wa umeme visiwani. |
Utekelezaji wa mradi wa nishati ya umeme jua unatakuwa wa awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza imeanza agosti 2016 na kukamilika desemba 2017, ambapo miundombinu imefikia hatua nzuri na visiwa vitakavyo nufaika na awamu hiyo ni Gana, Bwiro, Kamasi, na Bulubi. Katika awamu ya pili mradi utakamilika mwaka 2018 ambapo na kunufaisha visiwa vya Kweru kubwa, Kweru mto,Siza, Bushingere, Izinga na Sizu.
Ukaguzi wa miundombinu inayotumika katika mradi wa umeme jua |
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Frank S. Bahati ameshukuru Rex Energy kwa
kuwekeza nishati ya umeme jua katika visiwa kumi vya Ukerewe. Kupatikana kwa
umeme katika maeneo ya visiwa utasaidia kukuza uchumi hasa wa viwanda kwani ni
adhma ya serikali ya awamu ya tano kuwa na uchumi wa viwanda. Umeme utawasaidia
vijana kujishughulisha na kazi mbalimbali, pia mradi utakua msaada kwa
shule,vituo vya afya na taasisi za kidini. Amewataka wananchi kuupokea kwa
mikono miwili mradi na kushirikiana kuutunza kuhakikisha unakuwa msaada kwa
vizazi na vizazi.
Kikundi cha ngoma kikiburudisha katika uzinduzi wa umeme jua Gana |
Mkurugenzi
mkuu wa Rex Energy Francis Kibhisa ameshukuru Serikali kuanzia Wizara ya
Nishati na Madini, Rea na serikali ya Wilaya ya Ukerewe kwa kutoa ushirikiano
wa kufanikisha mradi huo kuanza kufanya kazi katika visiwa vya Ukerewe, baada
ya miezi miwili umeme utakuwa umewashwa. Baada ya mradi kuanza kazi kuna maeneo
ambayo itashirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuboresha maeneo makuu
matatu ambayo ni Elimu na kuimarisha majengo ya shule na vyoo kama ambavyo
wamesaidia ujenzi wa choo cha shule ya msingi Miti mirefu, Afya kuanzisha kituo
cha afya au zahanati, usalama kuweka kituo cha polisi.
Moja ya miundombinu ya mradi wa umeme jua kisiwa cha Gana |
“Gharama
za mradi ni bilioni 18 hadi 21 ambazo ni sawa dola milioni 9 hadi 11 za
kimarekani” alisema Kibhisa. Mradi utakuwa wa manufaa zaidi kwa vijana wengi
watapata mafunzo na kuajiriwa katika kazi mbalimbali za Rex Energy. Ametoa rai
kwa watanzania kuwekeza ndani ya nchi kama alivyofanya yeye na kuwa maendeleo
ya nchi yanaletwa na watanzania wenyewe na kutokata tama katika kusaidia
serikali.
Umeme
jua wa Rex Energy unatarajiwa kuwanufaisha wananchi zaidi ya 5000 na itavutia
wafanyabiashara wengi kutumia fursa na kujiongezea pato na wametakiwa
kushirikiana na mwekezaji kutunza miundombinu.
No comments:
Post a Comment