Wednesday, May 10, 2017

RC Mongella amewataka wadau kushirikiana kuboresha elimu Wilayani Ukerewe

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John V.K Mongela akizungumza katika mkutano wa wadau wa elimu Ukerewe, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Estominh Chang"ah, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ukerewe Frank Bahati, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. George Nyamaha(kulia kwa RC) 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amefanya ziara ya Siku tano (5) Wilayani Ukerewe kwa dhumuni la kukagua shughuli za Halmashauri na  miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa. Ili kuhakikisha sekta ya elimu inakua na mabadiliko ambayo yataleta ufaulu na mazingira mazuri ya wanafunzi kujifunza. Katika kuhakikisha hayo Mongella amefanya kikao na wadau wa elimu Wilayani Ukerewe ambapo amewaweka pamoja walimu wa kuu na wakuu wa shule zote, wenyeviti wa bodi za shule, maafisa elimu kata, maafisa tarafa, watendaji, wadau wa taasisi zisizo za kiserikali na wataalamu wa elimu ngazi ya mkoa katika ukumbi mkubwa wa mikutano wa Halmashauri.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John V.K Mongela akizungumza katika mkutano wa wadau wa elimu Ukerewe, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Estominh Chang"ah(kushoto kwa RC), Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. George Nyamaha(kulia kwa RC) 
Mongella amewaasa walimu kuwa na nidhamu ya kazi na uadilifu kwani wao ndio chanzo cha kuwa na maendeleo kielimu pia wawe mfano wa kuigwa. “bodi za shule ziwajibike na zisaidiane na uongozi wa shule kudhibiti nidhamu za watoto mashuleni” alisema Mongella. Amepiga marufuku kuunda tume kwa mwalimu atakae mpa mimba mwanafunzi na kesi za aina hiyo zisiwe za muda mrefu.
Amaewataka kuwepo na usimamizi madhubuti wa fedha za elimu bila malipo kwa shule zote za msingi na sekondari na fedha za serikali hizo zitumike kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo na kuahidi kuleta timu yakukagua fedha hizo na namna zilivyotumika na zinavyotumika na amewataka kurudisha hela kama mtu amezitumia vinginevyo. Lengo kuu ni kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora kutokana na fedha za elimu bure na historia inaonyesha ukerewe inauwezo mkubwa wa kufanya vizuri.
Wadau wa Elimu Wilayani Ukerewe
Mongella amezitaka kamati za shule na vikao vya wazazi vifanyike kila robo na visiishie kuchangishana bali wazazi wa elimishwe katika maeneo ya kitaaluma na wote wawajibike na taarifa na ratiba zipelekwe kwa Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella ametoa agizo juu wa ujenzi wa vyoo mashuleni ambapo amesema kufikia mwezi agosti 30 pasiwe na shule yenye upungufu wa matundu ya vyoo, na matundu ya vyoo katika shule yaende sawa na idadi ya wanafunzi na walimu katika shule husika. “bodi ya shule na mkuu wa shule ambaye hatakua amejenga choo itavunjwa” alisema Mongella. Pia amesisitiza bodi za shule na menejimenti za shule zihusike katika ujenzi wa vyoo.
Pia alisikiliza changamoto mbalimbali zinazowakabili katika kupeleka mbale elimu wilayani ukerewe na moja ya changamoto ni migogoro ya ardhi mashuleni hivyo akatoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanaanza mara moja upimaji wa ardhi katika shule ili kuepusha migogoro hiyo.
Mongella amewataka maafisa elimu kata wawajibike katika kufuatilia shule zilizopo katika kata yake na kuacha uzembe wa kutokutembelea shule. Wametakiwa kusisimamia mfumo wa elimu kwenye kata na watoto wote wanatakiwa kwenda shule waripoti mashuleni, na ametoa rai kazi kubwa ifanyike yakizalendo na hakuna kitakachotushinda. Amesisitiza elimu ni sekta nyeti tusaidiane tuisukume ili twende mbele na kufikia mafanikio.

Wadau wa Elimu Wilayani Ukerewe


No comments:

Post a Comment