Thursday, February 16, 2017

Uteketezaji wa Zana Haramu za uvuvi

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ukerewe Mhe. George Nyamaha akiteketeza zana za uvuvi haramu

Idara ya Uvuvi na Mifugo imeendesha zoezi lakukamata zana haramu za uvuvi ambapo imefanikiwa kukamata vitu hivyo ambavyo vimekuwa vikitumiwa katika uvuvi ambao umekua ukiharibu mazalia ya samaki na kupelekea kupungua kwa viumbe hao ziwani.
Moses Nduligu Mkuu wa idara ya Uvuvi na mifugo akifafanua jambo

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ametoa rai kwa wananchi wa Ukerewe ambao shughuli yao kuu yakujipatia kipato ni Uvuvi hivyo amewasihi kuachana na uvuvi haramu kwani ni mbaya na endapo watakamatwa watachukuliwa sheria kwa vitendo hivo. Ameyasema hayo alipokua akiongoza zoezi la uteketezaji wa zana hizo haramu kwa mazalia ya samaki na viumbe vyake.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ukerewe Mhe. George Nyamaha akiteketeza zana za uvuvi haramu


Zana zilizokamatwa na kuteketezwa katika shimo la taka la wilaya Bukongo ni makokoro ya sangara (bs) 5, makokoro vyambo/dagaa (ss) 13, nyavu za timba 173, nyavu za makila macho chini inchi6 zipo 15,kamba za kuvutia kokoro mita 2300. Zana hizi kwa ujumla zina thamani ya Tsh 75,040,000 .
Zana haramu zikiteketea Ukerewe.

No comments:

Post a Comment