Wednesday, April 5, 2017

Ulinzi na Usalama wa Mtoto

Wambura L. Kizito Mratibu wa Ustawi (M) akitoa mada wakati wa kikao kazi
Mtoto ana haki ya kulindwa na kutetewa pale anapotendewa ukatili ni wito uliotolewa na Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mwanza Wambura L. Kizito katika kikao kazi cha Ulinzi na usalama wa mtoto ambacho kimefanyika katika ukumbi wa hospitali ya Wilaya ya Ukerewe na kimewaweka meza moja wadau kutoka makundi mbalimbali wenye wajibu wa kumlinda mtoto kama maafisa ustawi, mwendesha mashitaka, hakimu mfawidhi, polisi, viongozi wa dini, NGO’s, wawakilishi wa watoto,idara ya maendeleo ya jamii, idara ya elimu msingi na sekondari na idara ya afya.
Washiriki wakisikiliza mada
Watoto hukumbana na ukatili mbalimbali katika maeneo mbalimbali wanapokuwepo, baadhi ya ukatili wanaokutana nao watoto ni pamoja na ukatili wa kihisia ambapo mtoto anakutana na matusi, kinyimwa chakula, kuto thaminiwa, ukatili wa kimwili inaambatana na vipigo,kukatwa viungo vya mwili, kuchomwa moto, kutumikishwa, ukatili wa kingono inahusisha kubakwa, kulawitiwa, kuguswa maeneo binafsi, kunajisi na ndoa za utotoni.
Wambura L. Kizito Mratibu wa Ustawi (M) akitoa mada wakati wa kikao kazi
Lengo la uwezeshaji ni kuhakikisha mtoto analindwa na Halmashauri inanafasi ya kuweka mifumo madhubuti ambayo itamtunza na kumthani mtoto na kufuata sera, kanuni na taratibu mbalimbali za kumlinda mtoto na zitasaidia kukabiliana na mila na desturi zisizo rafiki pamoja na rasilimali watu wenye mafunzo na uzoefu wa kutosha katika kumlinda mtoto.
Dkt.Titus Kaniki akichangia mada wakati wa kikao kazi
Kizito ameeleza huduma mbalimbali wanazohitaji watoto wanapofanyiwa ukatili ni pamoja na afya,matibabu, sharia, malezi, ushauri nasihi, elimu na ulinzi na amewataka wajumbe kuwahamasisha jamii kuwa walinzi wa watoto kwani mtazamo wa kijamii mtoto akifanyiwa ukatili mara nyingi anasemwa vibaya na wengine wanatengwa.
Wambura L. Kizito Mratibu wa Ustawi (M) akitoa mada wakati wa kikao kazi
Katika utekelezaji  Mahakama na jeshi la polisi wanapaswa kujengewa uwezo wa namna bora za kumhudumia mtoto kwani kuna hitaji kuangalia umri na jinsi yake. Hivyo wajumbe wote waliohudhuria mafunzo hayo wametengeneza timu ambayo itahakikisha usimamiaji wa ulizi na usalama wa mtoto, utoaji wa taarifa, elimu na uhamasishaji wa kumlinda na kumthamini mtoto dhidi ya ukatili.


No comments:

Post a Comment